“Mimi na Hamisa ni kama familia, namheshimu… ni msichana ambaye anajiheshimu na ninampenda,” Ali Kiba alijibu maswali ya Sound Brown wa Clouds Fm.
Aliongeza kuwa anamkubali Hamisa kwakuwa anajielewa na kwamba kwake kufanya kazi naye sio kitu kibaya.
“Watu waliweka dot kuwa kwakuwa Hamisa yuko Verde [Zanzibar] na Ali Kiba naye yuko Verde kwahiyo watakuwa wana-Verdeana, hapana. Ile ni hotel ya Kimataifa, na Hamisa ni wa Kimataifa na Ali naye ni wa Kimataifa kwahiyo watu wa Kimataifa walikutana,” aliongeza.
Kiba na Hamisa wanaonekana kwenye video ya ‘Dodo’, ambapo Ali Kiba anamuimbia mwali wake mwenye hadhi ya ‘Dodo’ la Kifalme, akimsimu mama yake kwa kumleta duniani na kumpa malezi.
Video ya wimbo huo imepata mapokezi mazuri ikifanikiwa kushika nafasi ya kwanza kwenye ‘trending’ ndani ya saa chache.
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE
No comments:
Post a Comment