Jaji wa Mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Phocus Mkeha, ambaye alikuwa akisikiliza maombi ya dhamana hayo amesema masharti ya dhamana hiyo kusaini bondi ya Shilingi Milioni 50, na mdhamini wake bondi ya Milioni 10, pamoja na kushikiliwa hati yake ya kusafiria.
Hata hivyo maamuzi ya utoaji wa dhamana hiyo ameyarudisha katika mahakama ya wilaya ya Shinyanga mahali kesi yake ya msingi ilipoanzia, ambapo wao ndio watasimamia masharti hayo.
Kesi ya Mbunge huyo wa Kishapu kwa mara ya kwanza ilisomwa Mei 8 mwaka huu katika Mahakama ya wilaya ya Shinyanga ambapo alisomewa mashitaka 12 ya uhujumu uchumi, kumiliki Silaha (Bunduki), na risasi kinyume na sheria.
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE
No comments:
Post a Comment