Inadaiwa kuwa mtu huyo ni raia wa Cameroon aliyewasili nchini humo kutoka nchini Ufaransa, ambaye aliingia nchini humo, juma lililopita na alikuwa amewekwa karantini, baada ya uchunguzi aliofanyiwa katika uwanja wa ndege wa Kinshasa na kubaini kuwa ameambukizwa virusi hivyo.
Kwa sasa anapatiwa matibabu katika kituo cha zamani cha kuwatibu wagonjwa wa Ebola, Mashariki mwa Mji Mkuu wa Kinshasa.
Ikumbukwe kuwa kisa cha kwanza cha mgonjwa wa virusi vya Corona nchini humo, kilithibitishwa siku ya Jumanne na Msemaji wa Wizara ya Afya, ambapo Congo ni nchi ya 11 barani Afrika, kuthibitisha maambukizi ya ugonjwa hatari wa COVID-19.
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE
No comments:
Post a Comment