Husika na kichwa cha habari hapo juu,
Kinachonisukuma kuomba ushauri hapa ni nyenendo za huyu mama na binti yake mmoja yule wa pili, yaani huyu mama anaforce mwanae nimuoe yaani niishi nae gheto kwangu niwe nalala naye na kuamka naye.
Kila chakula kikiiva naletewa nguo nafuliwa na hadi maji bafuni napelekewa na wanafanya yote haya si kwamba mimi nataka hapana ni kwa lazima, yaani chakula unaletewa ki nguvu nguvu kama ni wali unakuwa hadi ushamwagiliziwa maharage na mchuzi sasa kwa mazingira haya ni vigumu sana kukataa.
Jana binti kaja usiku kuniletea msosi na hakurudi tena ndani kwao akabaki hadi asubuhi, mimi leo nimeondoka kwenda kazini nimemuacha gheto nimerudi nimekuta kapika chakula chetu wawili tofauti na chao kile cha kwa mama yake.
Sasa kwa staili hii ya kuja gheto Jana usiku na leo nimemkuta kapika si tiari nishakabiziwa mzigo hivi.
Ushauri wenu nifanyaje? Nihame hii nyumba au nifanye nin?
LONDON BABY
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE
No comments:
Post a Comment