Mbunge wa Iringa mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa, amesema hoteli kubwa za Serena zimefungwa kutokana na ugonjwa wa virusi vya Corona.
“Hizi Serena ni hoteli kubwa zimefungwa. Hoteli moja unaweza kuwa na wafanyakazi zaidi ya 200 porini huko hakuna kabisa mtalii,” aliandika Mchungaji Msigwa katika ukurasa wake wa twitter.
Mchungaji Msigwa ni Waziri kivuli wa Maliasili na Utalii aliendelea kuandika kuwa
“@HKigwangalla liambie taiga what is up? Mr minister, don’t printed as if nothing is happening!,”
Katika tangazo lililitolewa na uongozi wa Serena hotel umeeleza kufunga hoteli zake za kitalii, Safari Lodge and camps na Hotel- Resorts kwa ajili ya kujikinga na Corona hadi Juni 15, 2020.
Hizi serena ni hotel kubwa zimefungwa
Hotel moja inaweza kuwa na wafanyakazi zaidi ya 200
Porini huko hakuna kabisa mtalii @HKigwangalla liambie Taifa what is up ? Mr Minister, don’t printend as if nothing is happening!
119 people are talking about this
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE
No comments:
Post a Comment