Zororo mtangazaji wa redio na runinga, alikuwa akitazamwa na wengi kama kipaji halisi kilichobeba nguvu na maono makubwa ya kihabari. Ni mtoto wa mfanyabiashara maarufu na Mbunge wa zamani wa ZANU-PF, James Makamba. Zororo alilazwa juzi Jumamosi katika Hospitali ya Wilkins mjini Harare, Zimbabwe hali yake ikielezwa kubadilika ghafla.
Amepata kuendesha vipindi mbalimbali maarufu kama State of the Nation, Point of View na kuongoza vipindi vya matukio katika ZiFM Radio. Hadi anafariki alikuwa na mkabata na serikali wa kufafanua masuala mbalimbali ya kitaifa kupitia video. Zororo Makamba alizaliwa Januari 17, 1990 na alikuwa msomi wa Shahada ya Kwanza ya Mawasiliano kwa Umma kutoka Chuo Kikuu cha Michigan nchini Marekani.
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE
No comments:
Post a Comment