Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Zuberi Chembela amesema kuwa jeshi hilo halijawapiga wanachana hao wa Chadema, akieleza kuwa wao wanapaswa kueleza waliowapiga.
“Jukumu la Polisi sio kupiga watu. Hao wanachama wa Chadema hawajapigwa na Polisi labda wawaseme waliowapiga lakini sio polisi,” Kamanda Chembela anakaririwa na Mwananchi.
Mdee na Bulaya waliepuka kifungo cha miezi mitano jela kila mmoja baada ya kulipiwa faini baada ya kukutwa na hatia katika makosa 12 kati ya 13 yaliyokuwa yanawakabili.
Wabunge hao walikuwa miongozi mwa viongozi nane wa chama hicho, ikiwa ni pamoja na Dkt. Vincent Mashinji aliyehamia CCM, waliohukumiwa kwenda jela au kulipa jumla ya Sh. 350 milioni kama faini.
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE
No comments:
Post a Comment