Siku chache baada ya Rais Yoweri Museveni kusitisha huduma za usafiri wa Umma ili kuzuia maambukizi ya #CoronaVirus, watu wawili waliokuwa wakienda kazini kwa kutumia bodaboda wamepigwa risasi na Polisi
Akizungumzia tukio hilo, Olyem amesema hakuangalia taarifa ya habari siku Rais Museveni alipotangaza hatua zinazochukuliwa kudhibiti #COVID_19 hivyo hakujua kama bodaboda zimepigwa marufuku
Ameeleza kuwa wakati wanaelekea kazini walizuiwa na Polisi walipojaribu kuuliza kosa walilofanya risasi mbili zilifyatuliwa hewani na baada ya hapo, Polisi wakaanza kuwapiga risasi
Hata hivyo, Msemaji wa Polisi Patrick Onyango, amedai wawili hao walipigwa risasi baada ya kujaribu kumshambulia Afisa wa Polisi
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE
No comments:
Post a Comment