Mashine hizo tatu zilizofungwa na hospitali ya Muhimbili zenye gharama ya Tsh milioni 210 na inatarajia kufunga mashine moja ya kusaidia mgonjwa kupumua (ventilator) yenye thamani ya TSh. Mil 56 katika Hospitali ya Rufaa Amana ili kuhudumia wagonjwa wenye maambukizi ya virusi Corona
MNH pia imefunga mtambo wa kuchuja maji (Portable RO) wenye thamani ya Tsh. Mil 28 na mtandao wenye miundombinu ya kusafirisha maji ili kuwezesha mashine hizo kufanya kazi ya kusafisha damu uliogharimu Tsh. Mil 12.
Aidha MNH inatarajia kupokea madaktari na wauguzi kutoka Hospitali ya Rufaa ya Amana kuanzia April 28, 2020 ili kujengewa uwezo kwenye Kitengo cha Kusafisha Damu pamoja na vyumba vya wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICUs) aina tano tofauti.
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE
No comments:
Post a Comment