Wizara ya Afya nchini Kenya imesema idadi ya watu walioambukizwa virusi vya Corona sasa imefika 320 baada ya leo kutangaza visa vipya 17, vilivyotokana na sampuli 668 zilizopimwa katika saa 24 zilizopita.Kati ya hao, 12 ni kutoka miji ya Mombasa na 5 Nairobi.
Wakati huo huo, Kenya pia imethibitisha kwamba wagonjwa 6 wamepona na kuruhusiwa kwenda nyumbani na kufikisha idadi ya waliopona nchini humo kufikia 89.
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE
No comments:
Post a Comment