Dereva Audax Ntebe amesema wamekosa Imani na zoezi la upimaji kwa kuwa hakuna tahadhari ya upimaji lakini pia hakuna uwakilishi wa Tanzania huku dereva Kassim Mkali akisema wakati wamezuiwa kuingia kenya, bado wanalipishwa ushuru wa maegesho kwa siku kiasi cha sh 4000 na fedha za ulinzi wa magari sh 3000 kwa siku jambo ambalo linaendelea kuwapa ugumu wa maisha.
Akizungumza na madereva hao, mkuu huyo wa wilaya, Mwaisumbe alisema tayari amewasiliana na mkuu wa wilaya ya Kajiado juu ya kupinga zoezi hilo ambalo amesema haliendi katika hali sahihi kutokana na kukosa uwakilishi kwa upande wa Tanzania.
Kufuatia hatua hiyo Mwaisumbe amesema kuanzia sasa magari na madereva kutoka kenya wanaoingia nchini, pia watatakiwa kupimwa na kusubiri majibu masaa 48 kama wanavyofanya wakenya.
HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE
No comments:
Post a Comment